Wasichana Waliojiunga Kikundi Cha Islamic State Waonekana

Kanda ya Video ya CCTV imeonyesha picha za wasichana watatu wa Uingereza waliotoroka nchini kwao  kuelekea nchini Syria ili kujiunga na wapiganaji wa IS.
Wasichana hao ambao ni  Shamima Begum,Amira Abase wenye umri wa miaka 15 na kadiza Sultana mwenye umri wa miaka 16 walisafiri kutoka London kuelekea Istanbul tarahe 17 mwezi Februari.
Picha hizo zimewaonyesha wakisubiri katika kituo cha basi cha Bayrampasa baadaye siku hiyo. Wapepelezi wa Scotland Yard wanaamini wanafunzi hao wa shule ya Bethnal Green Academy wameingia nchini Syria.
Inadaiwa kuwa  wasichana hao wamepelekwa karibu na kivuko cha mpaka huo na wapiganaji hao wa Islamic State. Katika kanda hiyo ya video Inaonyesha kuwa wasichana hao walikaa katika kituo cha basi kwa   kwa takriban saa 18.


Wasichana Waliojiunga Kikundi Cha Islamic State Waonekana Wasichana Waliojiunga Kikundi Cha Islamic State Waonekana Reviewed by Unknown on 12:25 PM Rating: 5

No comments

Comment to Cadotz

Ndugu ahsante kwa kuitembelea Cadotz, Endelea kufurahia huduma zetu pia Tunakusogezea Cadotz uchague unachokitaka katika menyu zetu.
Bofya chini

<<< rudi